Kikosi cha Simba sambamba na jopo la waamuzi kiliwasili mjini humo mishale ya saakumi na mbili asubihi kwa saa za Misri, sawa na saa moja asubuhi kwa saa za Afrika mashariki.
Kabla ya kuelekea mjini Port Said msafara wa Simba uliwasili Cairo Saa 7:50 usiku wa jana ikitokea Addis Ababa, Ethiopia ambako ilipitia kuunganisha ndege ikitokea Dar es Salaam, baada ya kuondoka jana jioni.
Baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Cairo, msafara wa Simba SC uliaanza safari iliyowachukua muda wa saa tatu kwa barabara kuelekea mji wa Port Said kwa basi maalum la kukodi.