Nguli wa soka nchini Argentina na ulimwenguni kwa ujumla Diego Maradona, amejitokeza na kumtetea Lionel Messi, kwa kusema mchezaji huyo hana haja ya kudhihirisha yeye ni bora katika mashindano ya kombe la dunia yatakayofanyika Urusi mwezi Juni.
Amesema hayo kufuatia kukusolewa na wadau mbalimbali wa soka kwa kushindwa kuisaidia timu ya taifa kwenye michuano mikubwa.