Header Ads

  • Breaking News

    BURUDANI: Mama Uwoya asema haitambui ndoa ya mwanae na Dogo Janja.













    Mama mzazi wa msanii wa filamu za bongo Irene Uwoya, Neema Mrisho amesema hampendi Dogo Janja kwa sababu msanii huyo hana adabu lakini pia amefunguka na kudai kuwa haitambui ndoa ya mwanaye Irene na Dogo Janja kwani ni ndoa ambayo imefungwa bila kufuata taratibu.
    Mama Uwoya amezungumza hayo leo, pindi alipokuwa anajibu hoja ya mwanae Irene aliyedai kuwa hadi leo hajampeleka mume wake nyumbani kutokana na sababu ya kuwa mama yake ni mtu wa kusafiri mara kwa mara hivyo bado wanatafuta muda wa kufanya jambo hilo.
    Mama Uwoya amezungumzia utetezi wa mwanaye kuwa hauna mashiko kwani hata kama anasafiri haiwezi kuwa mwaka mzima na kwamba, ukweli ni mtoto wake anajua wazi kuwa ndoa hiyo hawaitambui na hawamkubali Dogo kwa kuwa ni mtoto ambaye hana adabu.

    No comments

    Post Top Ad

    Post Bottom Ad